Katibu CCM Wilaya ya Ilala ahimiza viongozi kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo

http://raiatanzania.blogspot.com/2018/02/katibu-ccm-wilaya-ya-ilala-ahimiza.html
KATIBU wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ilala,
Joyce Mkaungala , amewataka Viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya shina hadi Wilaya
kuhakikisha wanachukua matatizo ya wananchi wao na kuyafanyia kazi kama ilani ya
chama inavyosema.
Akizungumza na waandishi wa habari leo mapema Ofisini kwake Ilala Boma ,Jijini Dar es Salaam,
Joyce, amewataka Viongozi kuachana na siasa uchwara na badala yake kuwatumikia
wananchi kutokana na mpangilio imara wa ilani ya chama na utekelezaji wake.
Joyce, amesema huu sio muda wa kucheza ni wakati wa
watendaji kutenda kazi kwa vitendo na kuhakikisha wanachukua jitihada mbali
mbali za kutatua kero za wananchi ili waendelee kujenga imani na chama hicho.
Amesema katika kuhakikisha kero za wananchi wa
Wilaya ya Ilala zinatatuliwa, wapo tayari kushirikiana na Uongozi wa ngazi za
juu ili kufichua uozo unaofanywa na
baadhi ya watendaji ambao si waaminifu wenye lengo la kutia doa Chama cha CCM
ambacho kinadhamira ya kumkomboa mnyonge na masikini.
![]() |
Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala, Joyce Mkaungala, (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari leo Ofisini kwake, kulia ni Katibu mwenezi wa CCM Wilaya ya Ilala Sultani Side |
“Sisi kama watendaji wa juu wa Wilaya tuna jukumu la
kuwakumbusha watendaji wa ngazi za Kata na Serikali za mitaa kupitia CCM katika
kutekeleza ilani ya Chama, hivyo tunawaomba viongozi wote wahakikishe kero
zinatatuliwa, wanachukua hatua madhubuti ili watu waendelee kukiamini chama
katika utendaji wake uliotukuka chini ya Rais John Magufuli ambaye ndiye
Mwenyekiti wa Chama”,amesema Joyce
Katika hatua niyingine, Joyce, amesema wapo kwenye
mkakati mkubwa wa kuhakikisha wanakutana na Wenyeviti wa Mitaa wote
waliochaguliwa kupitia tiketi ya CCM ili kuangalia ni kwa namna gani wataweza
kusaidiana katika kufanikisha maadhimio ya Chama na Ilani zinatekelezwa kwa
kiwango kikubwa na kuona chanagamoto ambazo zinawakuta na kuzifanyia kazi.
Pia, amesema hawafurahishwi na kauli mbaya
zinazotolewa na Upinzani huku akidai kwamba watu hao ni vibaraka wa Mabepari
na kauli za kiuchochezi zenye lengo la
kumchafua Rais John Magufuli, hivyo wanalaani kwa kauli moja na kuwataka wale
wenye kufanya hivyo vyombo vya usalama viwajibike kwa kiasi kikubwa katika
kuwaajibisha ili nchi iwe na amani kwani kuipoteza amani kunaweza kupelekea
machafuko makubwa
“Hatuwezi kuvumilia, kama hawa wanatumiwa kama
vibaraka wa Mabepari, hatutasita kuchukua uamuzi mgumu, tunahitaji nchi tulivu,
angalia Libya kipindi cha Gadaf na wakati huu mambo yakoje, wananyanyasika mlo
mmoja kwa siku, wazee na mababa zetu na watoto wanateseka, leo hii ikitokea
kwetu hata Machinga watashindwa kuweka mitumba yao sokoni , tuavipinga vitendo
hivi tunahitaji watu hawa washughulikiwe “ameongeza Joyce
Naye Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Ilala, Said
Sultan Side, amewataka Madiwani kuwajibika kwa wananchi wao na kufanya yale
waliyoyaahidi wakati wa kampeni ili kutimiza sera zao na kukitangaza vyema
chama cha Mapinduzi kwa kusimamia vyema Ilani ya chama.
Amesema kwa sasa pamoja na kuwa na changamoto
kadhaa, bado chama kinaendelea kuelimisha Vijana kuhusiana na gawio la asilimia
5 kutoka Halimashauri , hivyo amewataka wahusika kulegeza masharti katika kutoa
mikopo ili kila mtanzania na Kijana anufaike na keki ya Taifa kupitia Halimashauri
.
Pia ametoa wito na angalizo kuhusiana na Wenyeviti
wa Mitaa kuwatoza pesa Wananchi wanapohitaji huduma kwmba tabia hiyo
haikubaliki ndani ya CCM , hivyo kwa wale watakao bainika wanafanya vitendo
hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
“Nipende kuwaomba Viongozi acheni tabia hiyo, hata
kwenye kampeni Ilani ya chama chetu haikuelekeza hayo mambo, wito wangu kwa
wananchi kama mtawabaini viongozi hao tuleteeni majina yao tutawashughulikia ,”amesema
Sultani
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania, bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online