Mwenyekiti Mji Mpya aamuru soko kufunguliwa

http://raiatanzania.blogspot.com/2018/02/mwenyekiti-mji-mpya-aamuru-soko.html
MWENYEKITI wa Serikali ya Mtaa wa Mji Mpya Kata ya Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Justine Chiganga,
ameamuru soko la mtaa huo kuwa wazi ili wananchi wafanye biashara zao.
![]() |
Mwenyekiti wa Mji Mpya, Kata Ya Mabwepande, Justine Chiganga akizungumza na waanchi khusu mpango wa soko hivi karibuni |
Akizungumza na Raia Tanzania hivi karibuni ,
Chiganga, amesema , wananchi wanapata tabu sana ya kutafuta chakula hadi
kufikia kutoka nje ya mji jambo ambalo ni kero na kikwazo kwao.
Amesema, huduma ya chakula ni haki ya msingi, hivyo
kama huduma hiyo inasogezwa karibu wananchi hawatapata tabu tena ya kutembea
umbali mrefu kutafuta chakula.
Hata hivyo, Chiganga, amesema eneo hilo ni muda
mrefu lilikuwa tayari kutumika lakini kutokana na zuio la Manispaa ya kutokufanya kazi , lilikuwa
kikwazo kwao huku akida kwamba waliweka pingamizi hadi leo hawajatokea.
“Hili eneo tuligaiwa na Manispaa ya Kinondoni kama
watu wa kundi maalumu, chakushangaza baadae tulinyang’anywa na kuambiwa lina
utata kwamba kuna watu wanne ambao hawajulikani ndio wamiliki wa eneo hili”amesema
Chiganga

Aidha, Chiganga, amewataka wananchi kufungua eneo
hilo na kufanya shughuli zao kwani wao wana haki kama ilivyo kwa watu wengine.
![]() |
Baadhi ya wananchi wakikagua mandhari ya eneo la Soko la Mji Mpya ambalo limefunguliwa leo na Mwenyekiti Chiganga |
Naye mkazi mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe,
amesema wamechoka kula aina moja ya mboga hivyo kuwepo na soko eneo hilo
kutwasaidia kubadisha vyakula na watajipatia kipato kuppitia baishara zao za
ujasiriamali.
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania, bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online