ZIARA YA DC MJEMA, CHANGAMOTO YA ULINZI YAJITOKEZA KILA KONA


WAKATI ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Illa, Sophia Mjema, ikiwa imemalizika mara baada ya kutembelea baadhi ya miradi ya wananchi kwenye Jimbo la Ukonga, changamoto nyingi zilijitokeza lakini kubwa zaidi ni la ulinzi na usalama ambalo lilijitokeza kila kona.
Katika ziara izo, jumla ya Kata 13, zilitemebelewa ambapo kila kata kuiuwa na kikao cha mjuuisho wa wananchi kuelezea kero zao huku wakazi wengi wakiwa na shauku ya kutaka kujua ni lini watanifaika na miradi yao kwa ujumla.
Mkuu wa wilaya ya Ilala, katika ziara zake zote, suala la ulinzi na usalama liijitokeza kila kona, huku maagizo aliyoyatoa yakionekna kuwapa moyo na kuwatia faraja sana wakazi wengi waliojitokeza kwenye ziara hizo.
Akizungumza na waaanishi wa habari, jana kwenye ziara ya Kata ya  Msongola na Chanika, DC Mjema, alisema kuwa , suala la ulinzi ni la kil mtu licha ya kuonekana kupewa jukumu kubwa Askari.

Alisema kuwa, kama kuna wakazi wanawajua waharifu hao, wanatakiwa kushirikiana na viongozi wao wa Kata na Serkali za Mitaa ili suala hlo lipatiwe ufumbuzi wa haraka na kuhakikisha hali ya usalama ina kuwa shwari .


”Nimesikia kwamba wapo boda boda wanaokabwa, wengine wanauwawa na mnasema hamuwafahau, nitoe rai kwa wazazi, wakina baba na wakina mama, kama unamtoto wako unajua anajiuisha na ujambazi, kibaka, mkanye mara moja kwani tukimkamata sisi tutampiga sana, hivyo ni wajibu wenu kujilinda wenyewe na kuchunguzana”Alisema DC Mjema.

Akijibu hoja za wananchi kuhusu vijana wao wanaojihusihsa na boda boda  kukamatwa na polisi wakidai wanaonewa, DC Mjema alisema inaweza kuwa kweli wanaonewa na wengine wanakutwa na hatia, hivyo ametaka Jeshi la Polisi kanda ya Ukonga  wanapowakamata watu wasio na hatia wawaachie huru huku wenye makosa wapigwe sana.

Aidha, katika ziara hiyo ya jana, DC Mjema, alifanikiwa kutembelea  mradi wa Zahanati ya Mtaa wa Ruhanga, uliopo Kata ya Msongola wenye juma ya Vyumba 12 ambao unategemea kumalizika mwaka huu Oktoba wenye thamani ya shilingi Milioni 123  utakao hudumia jumla ya mitaa miwili ikiwamo Kiboga na Ruhanga.

Mbali na mrai wa Zahanati, pia alitembelea mradi wa Kisima Mtaa wa Mkera Kata ya Msngola, ambapo kisima hicho kina jumla ya Mita 150, takao hudumumia watu 1500 sawa na mita 5000 ambao una DP 3 katika mitaa 2, mnara mmoja  upo shule na mwengine utaudumia jamii na ukamilikaji wake unatarajiwa kuwa 30/10/2018

Katika hitimisho la ziara yake, pia alitembelea Kata ya Chanika na kufanikiwa kukutana na wananchi ambao walitoa kero zao na kuahidi kuzifanyia kazi na nyingine akizitatua papo kwa papo .
Miongoni mwa miradi ambayo alitemebelea Chanika ni pamoja na mradi mkubwa wa Stendi ya Mabasi, miradi  ya Elimu, Afya pamoja na Ulinzi na usalama na soko.

Related

habari 3075816423099607670

Post a Comment

emo-but-icon

item