KUMBILAMOTO AZIDI KUCHANJA MBUGA , KAMPENI ZAKE ZAWA GUMZO KILA KONA.
https://raiatanzania.blogspot.com/2018/08/kumbilamoto-azidi-kuchanja-mbuga.html

MGOMBEA
nafasi ya Diwani kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Omary Said
Kumbilamoto leo ameendelea na Kampeni yake ya pili kwenye hadhara ya Eneo la
Mtaa wa Butiama Kata ya Vingunguti katika kunadi sera zake kuelekea uchaguzi
mdogo wa marudio.

Kumbilamoto
ambaye alikuwa Diwani wa Zamani wa Kata hiyo kupitia CUF, amesema yeye kwa sasa
sio mpiga kelele bali Wananchi wa Vingunguti wanafahamu uwezo wake na
uwajibikaji kwa Wakazi hao.

Amesema
kuwa, moja ya mikakati amabyo ataifanya katika Sekta ya Usafiri ni pamoja na
Kuhakikisha Magari yanafika Katika Mtaa wa Butiama kwani mpaka sasa mazungumzo
na Mkurugenzi wa Mashkof yalishafanika kinachosubiriwa ni kuonana na Mkuu wa Wilaya
ya Ilalla pamoja na SUMATRA wakae meza moja wakubaliane ili kuondoa adha
wanazozipata wananchi wa Mtaa huo.

Katika
Upande wa Afya , amesema kuwa tayari ahadi zote alizozitoa kashazipatia
majawabu hivyo hana deni tena kilichobakia ni kero za Shule pamoja na Maji
ambapo amewahidi wakimchagua wakazi wa Mtaa wa Butiama watapata maji masaa
Ishirini na nne.

Hata
hivyo, amesema kuwa, Wageni wengi wanaingia Dar es Salaam wakifika wakitafuta
nyama weni wao wamekuwa wakiagiza kutoka Mikoa mingine, hivyo amesema Serikali
tayari ishatenga pesa za Kujenga Chinjio la kisasa litakalo kuwa likichinja
kuanzia Ngo’mbe 1000 kwa siku jambo ambalo litasaidia kuingiza pato Serikalini
na Kata yake .
Mbali
na ahadi hizo, amewahakikishia Polisi walopo kata yake kuwapelekea TV kubwa
(Flat Screen) pamoja na King’amuzi cha Azam TV ili wazidi kuona mazuri
yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya tano chini ya Rais Magufuli.
Pia,
amewaomba Wananchi waendelee kuwa na
imai nay eye kwani ana mategemeo makubwa ya kuifikisha Vingunguti mbali na
kuwaambia wawapuuze Wapinzania wanaoleta Propaganda dhidi yake.

“Nipende
kusema kuwa , mimi nawafahamu sana najua changamoto zenu zipo wapi, nilichelewa
kufanikisha kwa kuwa Chama nilichokuwa nacho mwanzo hakikutaka kushiriiana na
Serikali, sasa niwaombe radhi nmekuja nyumba kubwa tutatekeleza kwa vitendo
yale yote niliyo yaahidi na kukwama kwa kushirikiana na Wananchi wangu”Amesema
Kumbilamoto

Ikumbukwe
kwamba huu ni mkutano wa pili kuzinuliwa ambapo mkutano wa kwanza ulifanyika
Uwanja wa Msikate tama ambapo mgeni rasmi alikuwa Mwenyeiti wa UVCCM Taifa,
Kheri James na mkutano wa leo mgeni Rasmi ni Mwenyekiti wa Wazazi CCM Mkoa wa
Dar es Salaam , Ndugu Frank Kamugisha
Mkutano
mwengine utaendelea mpaka ratiba itakapo tolewa, na Uchguzi utafanyika Mwezi wa
9/16/2018 na siku ya Kufunga Kampeni ni Tarehe 15/9/2018.