Diwani Kumbilamoto atekeleza kwa vitendo agizo la Rais la Elimu bure


DIWANI wa Kata ya Vingunguti ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, leo  amekabidhi jumla ya Mikeka 20 ya kukalia Watoto katika Darasa la awali katika Shule ya Msingi Miembeni iliyopo Kata ya Vingunguti  Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuonyesha ni kwa jinsi gani anatekeleza agizo la Rais la elimu bure.
Akizungumza na Raia Tanzania Online, Kumbilamoto amesema kuwa msaada huo ni moja ya kuhakikisha Watoto hao wanaishi katika mazingira mazuri ya kusomea ili kusaidia kuinua Elimu katika Kata yake akiamini kwamba msingi mzuri wa Elimu unaanzia katika Elimu ya awali {chekechea).
Katika hafla fupi hiyo ya kukabidhi Mikeka, pia amepata fursa mbali mbali ya kukutana na Wazazi wa watoto hao na kuwashukuru sana Waalimuna Wazazi kwa umoja wao wanaouonyesha katika kukuza elimu za watoto hao.
""Nipende kuchukua nafasi hii kuwapongeza Waalimu wa shule hii kwa jitihada za kuwafundishi hawa hawa watoto, maendeleo yoyote duniani yanatokana na elimu bora, hata tunaposema tanzania ya viwanda lazima tutambue kwamba hatuwezi kuacha elimu nyuma, msingi wa elimu ni elimu ya awali, hivyo nipende kuwaomba wazazi na waalimu shirikianeni kwa pamoja kusongesha gurudumu hili la elimu mbele, kama wazazi mtakuwa pamoja na waalimu tuna imani tutatengeneza kizai bora chenye manufaa kwa kata yetu na taifa kwa ujumla, hiki ni kidogo nimebarikiwa nawaomba mkipokee tutazidi kushirikiana kwa kila jambo"" amesema Kumbilamoto

 Mbali na kutoa msaada huo, amesema jukumu la mzazi ni kuangalia maendeleo ya mtoto wake na wala si kumuachia mwalimu , maana kama waalimu watasusiwa jukumu hili tutawabebisha mzigo kmkubwa sana nilazima kila mzazi ajue maendeleo ya mtoto wake.

Amewaomba Wazazi wa kata hiyo kuhakikisha kila mtoto anasoma kwa vile Rais Magufuli ameleta elimu bure, hivyo hakuna sababu ya mzazi kumuweka mtoto wake nyumbani wakati elimu ni bure ,
Hata hivyo amewatakia Waislamu wote waliopo katika mfungo wa ramadhani, waingatie mafundisho yaliyotolewa katika kitabu cha dini huku akiwataka kumcha mungu na kuomba mazuri katika kipindi hiki hususani kumuombea yeye aweze kutimiza kile alichowaahidi wananchi wake.

Post a Comment

emo-but-icon

item