IYF yazindua mpango wa kumkomboa Kijana wa Kitanzania

TAASISI isiyo ya Kiserikali kutoka nchini Korea Kusini inayojishughulisha na masuala ya kuwajengea fikra na kuwasaidia Vijana kutoka Mataifa mbali mbali hapa nchini (IYF) , leo wamezindua programu ya Vijana ijulikanayo kama ‘Najivunia Tanzania kwa kazi za kujitolea Ng’ambo .



Uzinduzi huo  umefanyika kwenye Ukumbi wa Nkurumah ulipo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ulihuzuliwa na Vijana kutoka sehemu mbali mbali ikiwamo wanafunzi wa chuo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi mtendaji wa IYF kutoka  Makao Makuu nchini Korea Kusini, Prof: Seong Hum Kim, amesema lengo la mpangu huo ni kutaka kuona Vijana wa Kitanzania wakitumia fursa mbali mbali ili kuleta maendeleo ya nchi.
Amesema kuwa, Tanzania ni miongoni mwa Mataifa ambayo  yanawezza kuongoza Bara la Afrika kwa kuwa na Vijana wenye ualedi mkubwa juu ya mitizamo kuleta maendeleo na kufanya nchi hiyo kuwa moja ya Taifa lenye uongozi bora Afrika nzima.
Aidha, amesema kwa sasa Tanzania inakabiriwa na changamoto ya ajira hivyo kuzindua mpango huo wa kutembelea nchi mbali mbali kwa kazi za kujitolea utakuwa ni moja ya fursa kwa Vijana hao na kujitangaza Kimataifa kutokana na shughuli wanazo zifanya.
Image result for international youth fellowship

“Tunaipenda Tanzania, ni moja ya Mataifa ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi tumeona  ili kusaidia soko la ajira ni vyema tukawa bega kwa bega vijana hawa ili kufikia malengo yao na kukuza uchumi wa Taifa mbali na hayo tutapata Viongozi bora watakaoongoza kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni huku roho kubwa ikiwaongoza katika utendaji wao ni kuwa na hali ya kiuzalendo”, amesema Kim

Naye Mkuu wa program kutoka IYF hapa nchini, Prof: Jeong Hee Yong, amewataka Vijana kuangalia fursa na kuachana na dhana ya kuajiriwa kwani ajira zilizopo ni chache hazikidhi mahitaji ya Vijana wa Kitanzania wote, hivyo kama watabadili fikra na kuangalia upande wa pili anaimani watafanikiwa na kupelekea Taifa kuwa na uchumi imara kutokana na kuwa na wataalamu mbali mbali watakao saidia kukuza sekta za uchumi hapa nchini baada ya kupata maarifa kutoka nchi za nje.
Pia amesema mpaka sasa ni jumla ya Mataifa 80 yameomba watu wa kujitolea huku mpango wao kwa sasa ukiwa umefikisha jumla ya Mataifa 25 ambayo shughuli za taasisi hiyo zimekuwa zikifanyika ikiwamo Tanzania.
Image result for international youth fellowship

“Mwaka huu tunatarajia kuwa na Vijana 100 watao jitolea, tunachosubiria kwa sasa ni ratiba zetu na ni wapi Vijana watapangiwa ila idadi  ya Vijana itaongezeka  kadri ya mahitaji ”, amesema Yong


Hata hvyo kwa upande wa Afisa mahusinao ya Umma wa IYF, Mwazani Ramadhani aliyesafiri nchi mbali mbali ikiwamo Korea Kusini , amekiri kuwepo na fursa nyingi kwa Vijana watakao bahatika kujiunga na shirika hilo huku akiwataka Vijana wajitokeze kwa wingi kwani changamoto ya ajira Tanzania ni kubwa , hivyo kwa kufanya kazi za kujitole kutawasaidia kujenge mahusiano bora na Mataifa mengine.
“Tunaomba Vijana wajitolee, kuna Vijana wamejenga dhana ya kwamba kujitolea ni kupoteza muda jambo ambalo kwa IYF sio kweli bali utaweza kubadilisha fikra zako na kuwa na mtazamo chanya wa maisha”, amesema Mwazani

Kwa upande wa Mshauri wa Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam , Paulina Mabuga, amewataka Vijana wanyanyuke na wachukulie fursa hiyo kama ni ajira kwao kwa kufanya hivyo kutwaunganisha na Mataifa mbali mbali katika kujenga umoja na kutafuta fursa za ajira.

Amesema wameanzisha Klabu ya IYF chuoni hapo, na wanatarajia kuona matunda baada ya wanafunzi kujitolea kwani moja ya sifa itapelekea  kumjengea uwezo  uwezo mwanafunzi wa kupambana na mazingira tofauti inapofika suala la ajira.

“Hii ni njia bora kinachotakiwa ni Vijana kupambana, wenzetu nafasi kama hizi zinawajengea CV, hivyo tunatakiwa tukizipata tuzitumie kushiriki kikamilifu pengine tunaweza kushuhudia siku moja wimbi la ajira hapa nchini likapungua kwa kasi na tukapata viongozi imara na bora”,amesema  Mabuga

Ameupongeza Uongozi mzima wa IYF kwa kutambua umuhimu wa chuo chao na kufanya semina hapo kwani wanajua fikra Mlimani ni Chuo kikubwa ambacho kina beba zaidi ya maelefu ya wanafunzi ambao watakuwa mabalozi wa kusambaza ujumbe kwa wenzao kuhusiana na kazi za kujitoea.

Miongoni mwa shughuli zinazofanya na taasisi hiyo ambayo ina mipaka ya umri wa kujiunga kutoka miaka 18 hadi 35 ni pamoja na kusambaza tamaduni kutoka Mataifa mbali mbali, kukuza maendeleo ya rasilimali za nchi na kuziheshimu, kukuza uelewa na kubadilishana mawazo na mataifa mengine, kuhamasiha soko la ajira na kuhakikisha mtu anafurahia kujitolea kwa ajili ya kujenga mawazo mapya kwa maisha yake ya baadae.


JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania,  bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online

Related

habari 8448792271812359758

Post a Comment

emo-but-icon

item