British Council yatoa mafunzo kwa Walimu shule msingi na Sekondari nchini



Shirika la British Council nchini linawapatia mafunzo ya uongozi walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari ya siku tatu yanayofanyika katika Kituo cha walimu Mzimuni ambapo mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha na kuwaongezea  walimu hao uwezo wa kiungozi na kiutendaji pamoja na maarifa ya kiutawala kwa walimu wenzake anaowaongoza,wanafunzi, wazazi pamoja na jamii inayozunguka shule.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo Ofisa Elimu wa  Manispaa ya Kinondoni,Kiduma Mageni amelipongeza Shirika la British Council kwa kujitolea kutoa elimu hiyo ambayo walimu wakuu hao wakiizingatia na kuifanyia kazi kwa vitendo itawaletea matokeo chanya katika shule wanazozisimamia na kuwajengea heshima katika utawala wao pamoja na jamii nzima inayoizunguka shule hiyo.

“Kitendo cha British Council kujitolea kutoa mafunzo ya uongozi ya uwezeshaji kwa walimu wakuu wa shule za sekondari na msingi ni jambo zuri la kuwashukuru sana wanaongeza chachu ya kumsapoti Rais Dk.John Pombe Magufuli katika chagizo la kauli yake ya Elimu Bure hivyo basi ninyi walimu tumieni fursa hii mnayoipata kujifunza mengi katika semina hii na kwenda kuifanyia kazi katika shule zenu mnazoziongoza naamini kwa kutumia mafunzo haya mtaenda kubadilisha fikra hasi kuwa chanya katika shule zenu zitakazoleta matokeo mazuri ya nidhamu,morali kwa walimu wa kufundisha na ufaulu wa kiwango cha juu kwa matokeo ya wanafunzi wenu” Alisema Mageni

Aidha Meneja Mradi wa Connecting Classroom Bwana Ephraim Kapungu kutoka British Council ambao ndio wafadhili wa mradi huo amesema, British Council imekuwa ikifanya kazi na wizara ya elimu katika kuwajengea uwezo wa kiuongozi wakuu  wa mashule, mbinu bora za ufundishaji kwa walimu wa darasani, na kuwawezesha viongozi wakuu wa elimu wakiwemo watunga sera kuhudhuria mikutano mbalimbali ya kielimu ya kimataifa ili kujifunza na kubadilishana mawazo na viongozi wa nchi zingine.

“Sisi British Council kupitia mradi wa Connecting Classroom tumekuwa tukishirikiana na wadau wengine wa elimu pamoja na serikali katika kujengea walimu uwezo wa kuboresha na kutatua changamoto za kielimu zinazowakabili  wanafunzi wenye uhitaji maalumu ili kuhakikisha wanapata fursa ya kupata elimu bora inayoendana na uhitaji wao lakini pia kupitia mradi huu tumekuwa tukiwezesha na kufadhili urafiki wa kielimu kati ya shule za Tanzania na shule rafiki kutoka nchini Uingereza” Alisema Kapungu.

Nao wa wawezeshaji wa mradi wa Connecting Classroom Bw. Frank Mhando na Edwin Shunda wamesema kuwa kupitia mafunzo hayo wanawajengea uwezo walimu katika nyanja za uongozi bora wa mashule, mbinu bora za  kufundishia na ushirikiano wa kielimu ili kuwapa maarifa mapya walimu wapate mawazo mapya ya kuweza kuwasaidia katika uongozi na ufundishaji.

JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania,  bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online

Related

habari 7977599616259252056

Post a Comment

emo-but-icon

item