RC Makonda aridhishwa na kasi ya ukarabati Mabasi ya Jeshi

https://raiatanzania.blogspot.com/2018/01/rc-makonda-aridhishwa-na-kasi-ya.html
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salam, Paul Makonda, leo
ametembele mradi wa ukarabati wa Mabasi
yanayoendelea kufanyiwa marekebisho kwenye karakana ya Magari Mwandege,
Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani na
kuridhishwa na kasi na jitihada zao.
RC Makonda, amesema maendelo ya wananchi huletwa
na amani na usalama kama mahala patakuwa haukuna usalama ni vgumu kufikia
malengo .
Amesema kuwa , katika mabasi hayo yanayotarajwa
kumalizika siku za hivi karibuni yatakuwa na sehemu mbali mbali za kuchajia
simu, ambapo katika upande wa pembeni mwa basi na kwenye kochi zitawekwa sehemu
za kuchajia ili kuhakikisha Askari wote wanapatikana muda wote kwa nyakati
tofauti kutoa huduma kwa jamii.
Miongoni mwa lengo kuu la ukarabati huo wa mabasi
yapatayo 11, ni pamoja na kuhakikisha vyombo vyote vya ulinzi hapa nchini
ikiwamo Jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi, pamoja na Jeshi la Magereza
wanakuwa na ulinzi mzuri .
Pamoja na ukarabati wa mabasi hayo, RC Makonda
amehakikisha kuboresha gari la Matarumbeta
la Jeshi la Polisi kulifanyia ukarabati ili lionekane kwenye muonekano
mzuri.
RC Makonda, amewataka wale wote wenye kuhitaji
huduma za ukarabati wa Mabasi yao wasisite kwenda Dar Coach na watajionea
utofauti na hatimaye mabasi yao yatakuwa na taswira mpya.
"Napenda kuwahakikshia ukarabati unaendelea
vizuri, tunafanya hivi kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika mkoa wetu,
tunataka wananchi wawe salama pamoja na mali zao, tunategemea mwsihoni mwa
mwezi huu tutapata mabasi 5 na mengine 6 yaliyobakia kasi itaongezeka na
kuyapata yote 11 naomba na wengine wajitokeze kusaidia huduma nyingine ili maendeleo yazidi kukua kwa kasi
".Amesema RC Makonda
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Dar Coach, Manmeet
Lal, amesema ukarabai unaendelea vizuri, mpaka sasa kuna jumla ya mabasi 11,
huku mabasi 5 yakiwa ni ukarabati na 6 ni kwa ajili ya matengenezo mapya.
Pia Mkurugenzi huyo amesema jumla ya shilingi
milioni 830 za kitanazania zitatumika kufanya matengenezo hayo ambapo milioni
630 yatatumika katika matengenezo ya mabasi 6 na milioni 200 zitatumika
ukarabati wa mabasi 5
Naye Kaimu Kamishina wa Jeshi la Magereza (DCP),
Augastine Mboje, amesema ameridhishwa na utendaji wa Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda
kwa kazi nzuri anayofanya ya kuimarisha ulinzi na usalama kwa vyombo vyote hapa
nchini na kumtaka aendelee na moyo wa kujitolea
ili hali ya amani na usalama iwe na uhakika kwa wananchi.
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania, bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online
JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania, bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online