DC Hapi ataka chemba korofi, mitambo majitaka kufanyiwa kazi

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Ally Hapi, amewataka wale wenye majukumu ya kusimamia chemba korofi zote zilizopo Wilaya ya Kinondoni pamoja na Mitambo majitaka  wafanye kazi kwa bidii na kuwa wepesi kutembelea maeneo sugu ili kubaini maendeleo na kasi ya kazi iliyopo.
DC Hapi aliyasema hayo hivi karibuni  mara baada ya kutembelea maeneo yaliyo na shida ya Chemba korofi ambapo aliwataka Dawasa na Dawasco kuhakikisha kazi hiyo inakamlika kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha afya za Wananchi na kulinda miundombinu ya bara bara katika kuzuia upotevu wa pesa inayotumika kukarabati bara bara.
Akizunguma na Waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, DC Hapi alisema hafurahishwi na kasi ya maji taka iliyopo kwenye wilaya yake huku akiwataka wataalamu wanaosimamia miradi hiyo kuwa wabunifu wa kutatua matatizo kwa haraka na kuwa na majibu sahihi.

Aliwapongeza Dawasco na Dawasa kwa kazi nzuri walioifanya ya katika eneo la maji safi lakini hakuridhishwa na kasi ya kupambana na kuzuia maji taka yanayochangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira hivyo kuwaomba waongeze a kasi  kwenye upande wa kudhibiti  maji taka ikiwema kumaliza tatizo la chemba zote sugu.

Pia aliwapongeza Dawasa na Dawasco kwa jitihada walizozichukua za kuwa na eneo kubwa la Treatment Pond eneo la Kilonga Wima lililopo Jangwani Beach utakao gharimu kiasi cha dola za Kimarekani milioni 65 kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia , ambapo watajenga mtambo wa kusafisha majitaka utakao kuwa na uwezo wa kusafisha mita za ujazo 16,000 kwa siku na utajumuisha mfumo wenye urefu wa Kilometa 97 utakaopita eneo la Mbezi Beach, Kawe, Tegeta na maeneo mengine jirani.
Aidha alitoa muda wa mwezi mmoja Chemba korofi iliyopo eneo la  Mwenge iwe imekamilika na kila mradi uwe umemalizka ili kuokoa pesa za Serikali kupitia kodi za Wananchi.

Kwa upande wao, Kaimu Mkurugenzi Maji taka DAWASCO , Shabani Mkwanywe, alisema moja ya changamoto zilizopelekea DAWASCA ni uchakavu wa mifumo ya maji taka pamoja na mabomba mengi kuwa chakavu kutokana na kuwa na umri mkubwa huku akisema mengi yalitengenezwa kipindi cha miaka 1950-1970 huku wakazi wa Dar es Salaam wakikadiriwa kuwa laki tano tofauti na sasa kufikia takribani milioni tano.

Mkwanywe alisema mabadiliko ya upanuzi wa Jiji na maendeleo yake yamechangia kwa kiasi kikubwa kuwepo na chemba mbovu kwani Jiji limeendelea kila uchwao mijengo inazidi kuongezeka na huduma ya Chemba inazidi kuongezeka kwa kasi hivyo wapo katika kuhakikisha wanafunga Pump mpya ili kutatua tatizo.

Naye Kaimu mkurugenzi wa huduma za ufundi DAWASA, Modesta Mushi, alisema lengo la mradi wa Mtambo wa uchakataji Maji wa Kilonga wima ni kuongeza uwezo wa mfumo wa ukusanyaji wa Majitaka katika  Jiji la Dar es Salaam.
Alisema jumla ya kilometa 563 za mabomba ya ukubwa mbali mbali ya ukusanyaji majitaka , yatakusanya majitaka na kuyamwaga katika mitambo mikubwa mitatu itakayojengwa Mbezi, Jangwani na Kurasini.

Mushi alisema mitambo hiyo mipya itazalisha gesi asilia na umeme kwa ajili ya kujiendesha, hivyo kupunguza matumizi na gharama za umeme.

maji yatakayokuwa yamesafishwa yatauzwa na kutumika katika shughuli mbali mbali kama vile kupozea mitambo na umwagiliaji huku tope litakalo bakia baada ya mchakato huo litatumika kama mbolea kwa ajili ya kilimo pamoja na bustani za majani na miti ya kivuli na hivyo kupendezesha Jiji la Dar es Salaam.

“Mtambo huu utakuwa unauwezo wa kusafisha mita za ujazo 200000 kwa siku, mfumo wa mabomba yenye urefu wa kilometa 370 yatakayolazwa kuanzia Ubungo hadi Jangwani, Kinondoni, Mwananyamala, Msasani, kati kati ya Jiji na Ilala”Alisema Mushi


Awamu ya kwanza ujenzi wa mtambo utasafisha mita za ujazo 25,000 za majitaka kila siku na mabomba ya kilometa 17.43 yatakayojengwa katika mitaa ya Magomeni, pia katika awamu ya kwanza bomba linalomwaga majitaka baharini litaacha kutumika na badala yake yatakwenda kusafishwa katika mtambo huo ambapo jumla ya dola za Marekani milioni 90 zitatumika.

JIUNGE NASI , BONYEZA HAPA http://www.raiatanzania.blogspot.com ku-install App ya raiatanzania,  bila ya kuingia websiteTweet@Raia Tanzania online, youtube@Raia Tanzania online TV, Fb@Raia Tanzania online, insta@raia Tanzania online

Related

habari 7291619629602423158

Post a Comment

emo-but-icon

item