Mr. Nice afunguka bifu na Young Dee

MSANII aliyetamba  hapa nchini na kibao cha  Kikulacho,Mr. Nice  amefunguka mazito  huku akitishia  kumchukulia hatua kali msanii mwenzake  wa Bongo Flava  Young Dee.
Image result for mr nice
Mr. Nice, alimtuhumu  Young Dee kwa kitendo cha kutumia miondoko na mashairi ya wimbo King’asti  katika ngoma iliyotambulika kwa jina la kiben.

Hayo alizungumza  Kupitia radio Swahiba FM 102.9 ya Zanzibari, kwenye kipindi cha burudani cha Power Beat , ambapo Mr. Nice alifunguka  kuwa Young Dee hamfahamu wala kumtambua Young Dee.

“Hili suala sio jema sisi kama wasanii kuchukuliana milio sio vizuri, kuna utaratibu, kama angefuata utaratibu tusingefikia huku tunapotaka kwenda lazima tubadilike haki ya mtu haiuzwi”. Alisema Mr. Nice

Kutokana na tuhuma hizo, Mr. Nice, alipanga kumchukulia hatua kali kwasababu ya kuiba wimbo wake wa king’asti.


Related

burudani 4844655957239924596

Post a Comment

emo-but-icon

item