Meya Kinondoni ataka ukarabati wa kituo cha Afya Kigogo kuharakishwa

Meya wa Manispaa ya Kinondoni   Benjamin Sitta amemuomba mganga mkuu wa manispaa hiyo,kuharakisha ukarabati wa Jengo lililonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kituo cha  Afya  cha Kigogo jijini  Dar es Salaam, kukarabatiwa kwa haraka kwa lengo la kusaidia wananchi kupata matibabu kwa haraka ambao utagharimu kiasi cha shilingi milioni 46 .

Akizungumza na wadau mbalimbali waliouzulia katika hafla ya kukabidhiwa hati ya  Jengo, sitta amesema eneo hili limenunuliwa na serikali kutoka  katika kituo cha Dogodogo Center Street Children Trust(Caring for  our Childen)  kwa kiasi cha shilingi milioni 400.


Pia sitta amesema mahitaji katika sekta ya afya ni makubwa sana na hivyo serikali inajtahidi kupunguza bajeti kwenye vitu vingine na kuwekeza kwenye sekta ya afya ili wananchi waweze kupata huduma iliyo bora.

"Mahitaji ya wananchi wetu kwenye sekta ya afya bado ni makubwa sana ,lakini kigumu zaidi kwenye manispaa yetu ya Kinondoni tunaufinyu Wa ardhi wakuweza kujenga hospital kubwa Ila kwa kupitia kituo hichi kitaweza kuhudumia wananchi kutoka sehemu mbalimbali.


Aidha amesema   katika  manispaa hiyo wanategemea kila mtaa uwe na Zahanati na kila Kata kuwe na kituo cha afya ili kufanikisha huduma iliyobora kwa wananchi,pia  amesema wanategemea kujenga hospitali ya kisasa maeneo ya Magwepande ikiwa na lengo la  kupunguza msongamano katika hospitali ya Mwananyamala,sambamba na kujenga hospitali itakayofanana na huduma za hospitali  ya Apolo India ili kuweza kupunguza ongezeko la wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi.

"Tumefanya jambo kubwa sana,mategemeo yetu kila Mtaa uwe na Zahanati na kila kata kuwe na  Kituo cha Afya, ingawa tuna upungufu wa Zahanati  84, pamoja na vituo vya afya 18 na tumeanza mazungumzo  ya kujenga hospitali za kisasa itakayosaidia kupunguza wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje na kuweza kutibiwa hapa hapa  " Amesema Sitta.
Kwa upande wake Naibu Meya ambaye pia ni Diwani kata ya kigogo Mangalu Manyama,ameishukuru Serikali katika kufanikisha kununuliwa kwa Jengo hilo ambalo litakarabatiwa na  kujengwa kituo cha afya ili kuwasaidia wakazi wa kata ya kigogo kupata matibabu yaliyo bora


Hata hivyo Mganga mkuu wa manispaa ya Kinondoni Dk. Festo Dugange amesema katika halmashauri hiyo inatekeleza Adhima ya serikali ya kujenga Zahanati pamoja na Vitio vya Afya ili kuhakikisha huduma za afya zinaboreka katika jamii ambapo majengo waliyonunua kutoka Dogodogo Center yatasaidia wananchi kupata huduma kwa haraka Zaidi kutoka katika kituo cha Afya kwani Katika Zahanati ya kigogo inahudumia watu 66,654 kutokana na ufinyu wa majengo ya  huduma za afya.


”Majengo haya na eneo hili lililonunuliwa kutoka Dogodogo Center itasaidia sana kupunguza msongamano wa Wagonjwa katika Zahanati ya KIgogo kimsingi Zahanati inatakiwa isihudumie wagonjwa zaidi ya 5,000 lakini zahanati yetu inawahudumia wakazi wapatao 66,654 zaidi ya mara kumi na mbili ya uwezo wa zahanati" Amesema Dk. Dugange.



Related

habari 2737036975048318597

Post a Comment

emo-but-icon

item